Watu wawali wamefikishwa
katika mahakama ya wilaya ya Makete kujibu tuhuma za kugushi sahihi na kuandika
mhutasari wa kikao hewa na kuchukua zaidi ya shilingi milioni mbili katika
akaunti ya mfuko wa maendeleo wa kata ya Bulongwa wilayani Makete
Mwandishi wa www.francisgodwin.blogspot.com kutoka Makete , Edwin Moshi anaripoti kuwa ,Akitoa taarifa hiyo
kwa wanahabari ofisini kwake mwendesha mashitaka wa Taasisi ya kuzuia na
kupambana na rushwa (TAKUKURU) Bw. Frednandi Nsakuzi amewataja watuhumiwa hao
kuwa ni aliyekuwa diwani wa kata ya Bulongwa Estomin Mahenge na mwenzake Edwin
Swallo ambaye alikuwa mtendaji wa kijiji cha Bulongwa ambapo mpaka anafanya
tukio hilo alikuwa anakaimu ofisi ya mtendaji wa kata ya Bulongwa
Watuhumiwa hao
waligushi sahihi na kuandika mhutasari wa kikao hewa na kwenda katika benki ya
Nmb tawi la Makete na kuchukua zaidi ya shilingi millioni mbili kwenye akaunti
ya mfuko wa maendeleao ya kata ya Bulongwa wakidai kuwa ni kwa ajili ya ujenzi
wa shule ya sekondari Usililo ambapo mhutasari huo upo TAKUKURU
Watuhumiwa hao
walifikishwa mahakamani hapo jana kwa tuhuma hizo na walikana
mashitaka yanayowakabili ambapo kesi hiyo inatarajiwa kutajwa tena Machi
23 mwaka huu katika mahakama wilaya Makete na watuhumiwa hao wapo nje kwa
dhamana |
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni